Digg StumbleUpon LinkedIn YouTube Flickr Facebook Twitter RSS Reset

171 MWENYEZI Mungu ngome kuu

image_pdfsauvegarder en PDF-Saveimage_printImprimer-Print

 171

1. Mwenyezi Mungu ngome kuu, silaha ya imara! Katika shida na huzuni twategemea yeye. Mwovu akitukaribia kututia woga, akijithibitisha kwa hila na jeuri, tusimwogope yeye!

 

2. Kwa nguvu yetu tu dhaifu, na tungeshindwa hima, ila Mwenyezi yupo nasi, twaambatana naye. Ukitaka jina lake, ndilo Yesu Kristo; aliye mshindaji na mwenye mamlaka, Mfalme wa milele.

 

3.Na dunia yote ikijaa majeshi ya giza, tuliye naye Mungu wetu, hatutaona hofu. Mwovu amehukumiwa, hana nguvu tena ya kutuangamiza maungo wala robo; ashindwa na Mwenyezi.

 

4. Maneno yake Mungu wetu, tushikamane nayo! Hatushindii vya dunia, vya juu twatafuta. Tu hodari siku zote, hata hatarini; uzima twauweka kutii Mungu wetu: Ufalme una yeye.

M. Luther, 1528
A mighty fortress is our Gud, R.H. 431

No comments yet.

Leave a Comment