Digg StumbleUpon LinkedIn YouTube Flickr Facebook Twitter RSS Reset

170 NIKIONA shida huku katika safari

image_pdfsauvegarder en PDF-Saveimage_printImprimer-Print

170

1. Nikiona shida huku katika safari, Yesu aninong’oneza neno la faraja. Ananipa raha tele na furaha ya ajabu. Ninaandamana naye sasa na milele.

 

2. Tena njia ikienda juu ya milima, ninakaribia mbingu, nuru inaang’aa. Na katika nuru hii ninaona kwa uwazi nchi ya ahadi yake na urithi wangu.

 

3. Kwa imani ninaimba, hata hatarini, njia ‘kiwa ndefu huku, nitavumilia. Nyota za ahadi zake zinang’aa kwa usiku, zinaniongoza vema hata huko juu.

 

4. Kama Musa aliona nchi ya ahadi, kadhalika natazama nchi yangu juu; ninaisalimu sasa hwa uheri na imani. Natamani kufikako, kwa urithi wangu.

 

5. Vya hatari vikifika kati’ njia tena, Yesu yu pamoja nami, anichunga vema. Ninaendelea mbele, na mbinguni nifikapo nyimbo nzuri nitaimba na wakristo wote.

Werner Skibsted, Paul Ongman, 1930

No comments yet.

Leave a Comment