169 ASKARI wa imani sisi

169

1. Askari wa imani sisi, kwa shangwe tunaendelea, hata vita ‘kiwa kali tuna nguvu na ‘hodari. Tuna upanga wa imani, ni neno lake Mungu wetu; na kwa jina lake Yesu tunashangilia sasa.

Pambio:
Mbio tutaacha huku, vita ikiisha. Tutaingiamo mbingu ku starehe humo. Wao washindao huku, watapewa taji kwa mkono wa Mwokozi, anayewapenda.

 

2. Tuvae kila mtu sasa silaha zote zake Mungu. Na mishale ya shetani ‘tazimika mbele yetu. Tukimtii Bwana Yesu, twaendelea kwa ‘hodari, na kwa nguvu za ahadi tutakuwa washindaji.

 

3.Na ukipungukiwa nguvu, katika vita ukishindwa, Yesu atakutilia nguvu mpya ya kushinda. Kwa nyimbo za kushangilia, utahimili shida zote, na kupata kuokoa wenye dhambi na makosa.