168
1. Nina ushirika na furaha kubwa, namtegemea Bwana Yesu. Wingi wa uheri kwa waaminio: Kustarehe mikononi mwake!
Pambio:
Raha, raha, raha kwa Yesu na amani! Raha, raha, nastarehe mikononi mwake.
2. Raha ya ajabu ni rohoni mwangu, namtegemea Bwana Yesu. Nuru huangaza njia niendayo; nastarehe mikononi mwake.
3. Woga na huzuni zinatoka kwangu, nikitegemea Bwana Yesu. Ninafarijiwa siku zote naye, nastarehe mikononi mwake.
E.A. Hoffman
What a fellowship, R.S. 377; R.H. 482; MA.