166 TUKIENDA pamoja

 166

1. Tukienda pamoja, tukishikamana na Mungu, tunapata amani na raha; tukifanya daima yanayompendeza, yu karibu kutusaidia.

Pambio:
Raha, furaha twazipata kwa Yesu, tukidumu katika kuamini, kutii.

 

2.Ikiwapo dhoruba, na mawimbi ya’vuma, yanakoma kwa neno la Yesu. Tukiona jaribu na kuhofu adui, tutashinda kwa nguvu ya Yesu.

 

3. Tukibeba mizigo anatustarehesha, tunapata furaha halisi. Masumbuko yatoka, giza inageuka kuwa nuru njiani mwa Mungu.

 

4. Tuna raha ya Mungu katika mashindano tukitii na tukiamini. Jua lake la pendo linawaangazia watiio na waaminio.

J.H. Sammis