164 IZRAELI wake Mungu

164

1. Israeli wake Mungu, kimya sana, wa’zunguka Yeriko kwa imani. Malaika wake aliwaongoza, na waliendelea kwa kushinda.

Pambio:
Twende kwa kushinda, twende kwa kushinda! Kwa damu yake Yesu, twende kwa kushinda! Tegemea Mungu, anatuongoza, na kwa imani, twende kwa kushinda!

 

2. Na Daudi, mchungaji, alikwenda mbele yake Goliathi bila woga; kwa imani alitupa jiwe lake, kwa jina lake Mungu akashinda.

 

3. Danieli aliomba kila siku, hakuhofu pango la simba kamwe; katika imani aliomba Mungu, akaokoka katika hatari.

 

4. Hata safarini huku kwenda mbingu nikipita katika jangwa kavu, na kupatwa na ‘jaribu mbalimbali, najua kwa imani nitashinda.

 

5. Na imani inashinda hali zote, inaruka juu ya mambo yote. Niliye dhaifu sitahofu kamwe, kwa kuwa Mungu ananiokoa.

William Grum