Digg StumbleUpon LinkedIn YouTube Flickr Facebook Twitter RSS Reset

163 AHADI zote za Mungu zinasimama kweli

image_pdfsauvegarder en PDF-Saveimage_printImprimer-Print

163

1. Ahadi zote za Mungu zinasimama kweli, na zilitiwa muhuri kwa damu yake Yesu.

Pambio:
Mbingu zikiondoka, nchi ikitoweka, ‘aminiye ‘taona: Ahadi zinadumu.

 

2. Fanya kama Ibrahimu: Uangalie juu! Nyota ukizihesabu, imani itaota.

 

3. Katika giza njiani tutaamini tu. Muda kitambo, na tena jua litaangaa.

 

4. Watu wakitusumbua, tutaamini tu. Yesu atusaidia majaribuni pote

 

5. Rafiki wakituacha, tutaamini tu. Yesu, rafiki mkubwa, atabaki daima.

 

6. Katika mambo yo yote tutaamini tu. Tutaviona mbinguni tulivyoviamini.

Lewi Pethrus, 1913

No comments yet.

Leave a Comment