162 Bwana Yesu

 162

1. Bwana Yesu, uwe nami, bila wewe nina hofu, unikaribie sana, uwe kiongozi wangu!

Pambio:
Sitaona hofu tena, Yesu Kristo yu karibu. Ninataka kufuata njia yako siko zote.

 

2. Bwana Yesu, uwe nami, kwani mimi ni dhaifu; na unifariji moyo kila siku ya huzuni!

 

3. Bwana Yesu, uwe nami siku zote safarini, zikiwako shida huku au raha na amani!

 

4. Bwana Yesu, uwe nami! Nahitaji nuru yako hata nitafika mbingu, kao letu la milele!

Fanny Crosby, 1884