160 AHADI zote za Mungu wetu zanasimama hata milele

160

1. Ahadi zote za Mungu wetu zinasimama hata milele. Milima yote ikianguka, ahadi hazipunguki.

Pambio:
Ahadi zake zinasimama, hazipinduki hata milele. Ikiwa nyota zingezimika, ahadi zake zinadumu.

 

2. Ahadi zake zinasimama katika shida, katika giza. Na nikichoka kwa vita kali, ahadi hazipunguki.

 

3. Ahadi zake zinasimama katika homa, katika kufa. Nafarijiwa na Baba yangu, ahadi hazipunguki.

 

4. Ahadi zake zinasimama; nitaamshwa katika kufa. Kwa Baba nitapokea taji; ahadi hazipunguki.

Johan Holmstrand, 1924