16 YO YOTE uonayo huku katika mwendo wako

16

1. YO yote uonayo huku katika mwendo wako, Yafaa kumwambiya Yesu atakusaidia.

Refrain:
:/: Kwa kuwa kila aombaye Mwokozi ne’ma yake, ataokoka na hatia, na atasifu Yesu. :/:

2. Ukichukiwa na wenzake na ukijaribiwa, Mwokozi yu karibu sana, Maombi asikia.

3. Ukiwa mwana mpotevu, na mbali na Babako, Amani una’kosa sasa, Urudi kwake Yesu!

4. Ukiwa na makosa mengi, Na roho yako ngumu, Neema yake yakutosha, utubu dhambi zako

5. Ikiwa nguvu mara nyingi kuomba kwa bidii, uombe Baba, kama mwana, akusikia kweli!

Carl Lundgren


[youtube https://www.youtube.com/watch?v=ZR8mfMstQws?feature=oembed&w=500&h=281]