157 HAIDURU kwangu uku chini

157

1. Haidhuru kwangu huku chini utajiri au umaskini, ila Bwana Yesu awe nami; ninatunzwa naye siku zote.

 

2. Haidhuru kama ninakuta shida nyingi katika safari, ila Mchungaji wangu mwema anilide na kuniongoza.

 

3. Haidhuru kama tunakaa katika baridi au hari, kwa sababu ukombozi wetu unakaribia. Haleluya!

 

4. Haidhuru kama sitapata utukufu na heshima huku; nikifanywa kama takataka, yanipasa kupendeza Bwana!

 

5. Haidhuru kama njia yangu inanichokesha mara nyingi, basi, nisigombane na ndugu, na pamoja tutashangilia!

 

6.Haidhuru kama tukiona sisi si wakubwa huku chini. Tuwe watumishi wake wema, na tutaingia kwake Bwana!

 

7.Haidhuru kama twasafiri katika dhoruba ya bahari, kwani Yesu ni nahodha wetu, atatufikisha bandarini.

Jonas Andersson