154 E’RAFIKI shaka zako zipeleke kwake Yesu

154

1. E’rafiki, shaka zako zipeleke kwake yesu!
Aliyemwamini yey hataona haya kamwe.

Refrain:
Naamini, naamini, ninakuamini, yesu. Naamini, naamini, naamini neno lako

2. Dhambi zote ziungame na kwa damu utakaswe,
akuvike haki yake! Atakufikisha kwake.

Refrain:
Naamini, naamini, ninakuamini, yesu. Naamini, naamini, naamini neno lako

3. Masumbuko yako yote uyaweke mbele yake!
Ukipita uvulini, bwana yesu yupo nawe.

Refrain:
Naamini, naamini, ninakuamini, yesu. Naamini, naamini, naamini neno lako

4. Na furaha yako pia ijulike kwake yesu,
yeye bwana ju’ ya yote akubarikie yote!

Refrain:
Naamini, naamini, ninakuamini, yesu. Naamini, naamini, naamini neno lako

5. Ujitoe kwake yesu: roho, mwili na akili vyote vya
maisha yako anataka ku’takasa.

Refrain:
Naamini, naamini, ninakuamini, yesu. Naamini, naamini, naamini neno lako