153 YESU CHRISTO alifufuka

153

1. Yesu Kristo alifufuka, akatoka kaburini. Furahini na msifuni, kwani alishinda kufa!

Pambio:
Habari njema: Alifufuka katika wafu! Yesu yu hai, naye atakuja tena.

 

2. Nguvu za mauti na dhambi Yesu Kristo alishinda; nasi sote tutashinda kwa nguvu yake ya ajabu.

 

3. Kundi dogo, msiogope, Bwana Yesu ni uzima! Aliziondoa dhambi na anawafariji moyo.

 

4. E’ wakristo, shangilieni, Yesu aliyefufuka yu karibu, atakuja na atatufufua sote!

Eric Bergqvist, 1904