Digg StumbleUpon LinkedIn YouTube Flickr Facebook Twitter RSS Reset

150 NATAKA kupokea baraka yake Mungu

image_pdfsauvegarder en PDF-Saveimage_printImprimer-Print

1. Nataka kupokea baraka yake Mungu, nataka kubatizwa kwa Roho ‘takatifu. Ju’ ya ahadi yake napumzika sana, aliahidi mimi kupata Roho yake.

Pambio:
Sawa na bahari, sawa na bahari ni neema yake anileteayo. Anayenijaliza, anayeniponyesha, ni Mwokozi wangu. Asifiwe sana!

 

2. Kanisa lake Mungu linaipata mvua, vijito vya baraka vinamiminwa sasa. Furaha ya uzima ni kubwa kati yetu. Tuimbe haleluya! Tumshukuru Yesu!

 

3. Mawimbi ya wokovu yanatujia sasa. E’ Mungu, tunaomba: Ujaze sisi sote! Watakatifu wako watakasike sana! Tuimbe haleluya! Tumshukuru Yesu!

 

4. Mawimbi ya wokovu yaliyofika kwetu, E’ Mungu, uyatume ulimwenguni mwote, maelfu kati watu wapate kuokoka, waimbe haleluya, wamshukuru Yesu!

H.J. Zelley, 1900
Like a mghty sea

No comments yet.

Leave a Comment