15 MUNGU moto wako uniutumie

1. MUNGU, moto wako uniutumie, Ninangoja nguvu yako! Nipe na uzima na upendo wako, Unijaze, E’Mwokozi wangu!.

 

2. Teketeza usiyopenda, Nisafishe kati’ damu! Na karibu yangu uivunje tena, unionyeshe, Yesu, niwe safi.

 

3. Unilinde, Yesu sikuasi tena unifunge kwa pendo! Mimi ni dhaifu, unitunze kwako ‘uniongoze kwa mkono wako.

 

4. Huko juu kwako tutaona raha, na huzuni itakwisha. Nyimbo za shukrani zitajaza mbingu; utukuzwe, Yesu, Mkombozi