Digg StumbleUpon LinkedIn YouTube Flickr Facebook Twitter RSS Reset

147 MWENYEZI Mungu wazamani

image_pdfsauvegarder en PDF-Saveimage_printImprimer-Print

1. Mwenyezi Mungu wa zamani zote ni kimbilio la vizazi vyote. Katika vita anawashindia na ku’okoa watu wake wote.

Pambio
Mfalme ‘kubwa ndiye Mungu, vitani anatushindia. Kwa shangwe kubwa tumsifu na tumwimbie Mungu wetu!

 

2. Mwenyezi Mungu wa zamani zote aliokoa watu utumwani, kwa njia kavu katika bahari wakafikishwa ng’ambo kwa salama.

 

3. Mwenyezi Mungu wa zamani zote Karmeli alishinda yule Ba’li, akasikia ombi la Eliya, ‘katuma moto juu ya sadaka.

 

4. Mwenyezi Mungu wa zamani zote akawa naye Daudi vitani; aki’tupia jiwe Goliati, shujaa alikufa mara moja

 

5. Mwenyezi Mungu wa zamani zote, uovu wote utashindwa naye. Atamseta yule mdanganyi, shetani, chini ya miguu yake.

 

6. Mwenyezi Mungu wa zamani zote atuongoza kwa mikono yake; anatulinda hatarini huku, mbinguni tutafika kwa salama.

No comments yet.

Leave a Comment