146 KARIBU nawengu nilipotea njia

1. Karibu na wenzangu nilipotea njia, rohoni mwangu njaa, na sikuona raha, lakini sasa Yesu ni Mchungaji wangu, naandamana naye siku zote.

 

2. Katika shamba lake nimefuata Yesu, ninapajua anapolisha kundi lake. Na penye maji hai napunzika sana, naona raha hapo siku zote.

 

3. Lakini mchungaji apita vitu vyote, uzima aliweka kwa ‘jili ya kondoo. Nikumbukapo Yesu, sioni tena kitu cha kupendeza ila yeye, Bwana.

 

4. Naimba kwa furaha rohoni mwangu hivi: « Upendo wako, Yesu, ninausifu sana!» Na jina lake Yesu ni kama manukato; ananilinda vema siku zote.

Lewi Pethrus