145 MUNGU wangu mkuu

1. Mungu wangu mkuu, wanijaza mwenyewe, na uzima u katika wewe. Nina raha moyoni na amani halisi, ninaishi katika upendo.

 

2. Sasa ninakusifu wewe, Yesu Mwokozi, unakaa rohoni daima. Kila ‘nachohitaji wanijaza kwa pendo. Wewe yote, na mimi si kitu.

 

3. Jina lako ni pendo, kulijua hakika kunafanya safari nyepesi. Mimi mtu dhaifu, ila kwako ni nguvu; niongoze katika safari!

 

4. Mbele ya uso wako giza yote yatoka; nuru inaangaza moyoni. Yamepita ya kale, sasa yote ni mapya. Ni maisha ya heri ajabu!

 

Joseph Gulseth, 1901