143 HERI alisi

1. Heri halisi, Yesu ni wangu! Yeye mchunga, mimi ni wake. Heri yakini, yote ni heri, roho na moyo zimeokoka.

Pambio:
Yesu ni wimbo na raha yangu, nitamsifu hata milele! Na nitamwona huko mbinguni. Yesu ni wangu na mimi wake.

 

2.Nilijitoa kwa Bwana Yesu, na nilipewa wokovu wake. Huko mbinguni kuna furaha juu ya mtu aliyetubu.

 

3. Sasa naweza kusifu Yesu, na roho yangu inafurahi. Mimi si kitu mbele ya Mungu, bali ni heri. Namshukuru!

 

4.Nimebatizwa katika Roho, shangwe ya mbingu imo rohoni. Moto moyoni, pia kinywani, nashuhudia pendo la Mungu.

 

Fanny J. Crosby – Van Alstyne, 1873
Blessed assurance, R.S. 417

[youtube https://www.youtube.com/watch?v=GwjZWPdhS_U?feature=oembed&w=500&h=281]