14 MWOKOZI wangu ulikwenda juu kukaa kuumeni kwake Baba

1. MWOKOZI wangu ulikwenda juu kuumeni kwake Baba;

Utakusanya sisi sote huko, Mbinguni kwako utatufikisha.

:/: Makao mema wa’tulinda, Unatungoja kwake Mungu Baba. :/:

 

2. Mwokozi wetu wewe, Yesu Kristo, kwa’ajili yetu mbele yake Baba.

Wachungu sana sisi, kundi lako, Na watusaidia ‘jaribuni.

:/: Na sikuzote unatuombea, watushindia vita kaili huku. :/:

 

3. Mikono yako uliwanyoshea walio wako, siku uli’kwenda;

Na hivyo siku utakaporudi utabariki wakuaminio.

:/: Ulivyokwenda, utakavyorudi; Niombe, nikakeshe kwa imani!:/: