139 NINAFURAHA kubwa

1. Nina furaha kubwa, napumzika sana, kwa kuwa nimefika kwa Mungu, Baba yangu. Ameniweka huru na mbali na utumwa, na sasa nakaa salama.

 

2. Zamani nilidhani kuacha dhambi zote, lakini sikuweza kushinda peke yangu. Ninamwamini sasa Mwokozi wangu, Yesu, na yeye ananishindia.

 

3. Mwokozi wangu, Yesu, aliyenifilia, aliokoa mimi, angali anipenda; nahesabiwa haki katika damu yake, inayosafisha kabisa.

 

4. Na nikijaribiwa na mwili wangu tena, ninakumbuka Yesu, apita vitu vyote. Neema yake kubwa kuliko dhambi zangu. Ninamshukuru Mwokozi.

 

5. Na sasa Bwana Yesu akaa ndani yangu, neema yake kubwa yanizunguuka mimi. Sitasumbuka tena, nimejiweka kwake, na Mungu anilinda vema

 

6. Shetani akitaka kufanya vita sasa, sitaogopa yeye na mamlaka yake. Maneno yake Mungu, ni yenye nguvu sana kwa wote wanaoamini.

 

7. Ninaenenda sasa kwa jina lake Yesu, salama nitafika nyumbani mwa Babangu. Lakini safarini naimba siku zote, nikimshukuru Mwokozi.

Nils Frykman, 1881