138 SASA tayari kwetu siku yakuokoka

1. Sasa tayari kwetu siku ya kuokoka, Yesu alitimiza yote msalabani. Wengi wanamjia Yesu Mwokozi wao, wapate kustarehe, wapone nafsi zao.

Pambio:
Mwana-kondo’ wa Mungu tunakusifu sana! Uzima uliweka kwa’jili yetu sisi. Umetufanya kuwa mitume yake Mungu. Kati’ majina yote lako ni kubwa mno.

2. Wewe kwa damu yako ulikomboa sisi, na jua la neema linatuangazia. Tumefahamu sasa pendo la Mungu wetu. Damu imetuunga kati’ agano jipya.

3. Njoo upesi nawe uliyesitasita! Mungu atakujaza neema yake kubwa, raha rohoni mwako inayokutuliza, matumaini, nguvu, pendo lililo bora.

H. Schlager, 1925
Speak to my soul, Lord Jesus, R.S. 567