134 WETU wa Mungu

1. Watu wa Mungu, mshangilieni kabisa, na mwimbieni Mfalme wa mbingu na nchi! Mungu yu nasi kwa pendo kubwa, kamili ili tupate wokovu.

 

2. Ona ajabu! Mwokozi aliyejidhili! Pendo kamili na neema nyingi ya Mungu: Alizaliwa, akawa mwana Adamu, atukomboe na dhambi!

 

3. Sisi wakristo tumwimbie tena pamoja Yesu Mwokozi aliye dhabihu ya kweli! Na atukuzwe hapa na huko mbinguni, kwani alitufilia!

 

4. Yesu Mfalme, kwa pendo uliniokoa, nikufuate, nikutumikie daima! Huko mbinguni nitakusifu milele katika watakatifu.

G. Tersteegen, 1735