133 UFURAHI moyo wangu
1. Ufurahi, moyo wangu, heri nyingi umepata!
:/: Sikitiko limekwisha, Yesu ni wangu nami wake. :/:
2. Ameponya roho yangu, yeye ni mponyaji mwema;
:/: Na kwa Roho ‘takatifu anabatiza watu wake. :/:
3.Jina langu ni mbinguni, Yesu ameliandika.
:/: Mimi mali ya Mwokozi hata milele na milele.:/:
4.Na moyoni mwangu sasa ninaimba: Mungu, Baba!
:/:Ni furaha kubwa sana, nina rafiki kila saa. :/:
5.Nimeondolewa dhambi, nisitende ovu tena!
:/: Kwani Yesu aokoa kila wakati na dakita. :/:
6.Nyimbo za kusifu Mungu zinajaa mbingu zote.
:/: Moyo wangu unajibu: Amina. Mungu asifiwe» :/:
Emil Gustavsson, 1887