132 YESU mwokozi unanipenda

1. Yesu Mwokozi, unanipenda, na pendo lako ni kubwa kabisa. Ulinivuta karibu nawa, Mimi ni wako daima dawamu.

 

2. Yesu Mwokozi, unanipenda, na pendo lako lapita akili. Linanifunza kuzifahamu raha, upole na utu adili.

 

3. Yesu Mwokozi, unanipenda, mimi maskini, dhaifu, mnyonge. Nimetakaswa kwa damu yako; ninakuomba, ‘nijaze upendo!

 

4. Yesu Mwokozi, unanipenda, umenitilia wimbo kinywani wa kukusifu hata milele, nitakuona halisi mbinguni.