125 HALELUYA! nafurahi

125

1. Haleluya! Nafurahi, ninaimba kila siku sifa zake Mungu wangu, aliyeniweka huru. Haleluya! Bwana Yesu aliniokoa kweli! Haleluya! Mimi wake, yeye ni Mwokozi wangu!

 

2. Heri! Nilieokoka kwa neema yake kubwa ninataka kumsifu Mungu na wokovu wake. Wakinung’unika wote, sitawafuata wao; nitasifu Mungu wangu siku zote na milele.

 

3. Kama ndege waimbavyo asubuhi bustanini, Na sauti ya mawingu ivumavyo baharini, hivyo nitamshukuru Bwana wangu kwa furaha. Roho yangu itaimba: Haleluya! Sifu Mungu!

 

4. Haleluya! Furahini mbele yake Mungu wetu! Na watakatifu wote, mwimbieni jina lake! Malaika wote pia, ……msifuni Bwana Mungu! Mbingu zote zitajibu: Haleluya, Haleluya!

Einar Karlsson, 1917