122 MWOKOZI kamili ni Yesu pekee

122

1. Mwokozi kamili ni Yesu pekee, Mwokozi mzuri halisi. Katika wokovu wa Mungu mkuu ninalindwa naye kabisa.

Pambio
Katika wokovu nalindwa salama, naishi kwa maji ya ‘hai. Upendo wa Mungu unanizunguuka :/: na kanihifadhi daima. :/:

 

2. Baraka ya mbingu inanijaliza kwa Roho ya utakatifu. Nasifu Mwokozi katika furaha, wokovu umenifikia.

 

3. Mwokozi mzuri ni Yesu pekee, aniondoaye mizigo. Njiani ananiongoza vizuri, anipa na nguvu ya mwendo.

 

4. Nitakapomwona Mwokozi mbinguni baada ya shida za huku, Nitamhimidi na kumshukuru Bwana ninayempenda.

Fanny J. Crosby, 1903