120 MSALABANI nilimuona Yesu

120

1. Msalabani nilimwona Yesu, Mwokozi wangu aliyeniponya; rohoni mwangu giza ikatoka, ninafuata Yesu sasa.

Pambio:
Nimeokoka kutoka dhambi, na siku zote ninaimba kwa furaha. Ni vita kali kushinda yote, lakini Yesu yu karibu.

 

2. Mwokozi wangu ananipa nguvu, nikiuona udhaifu huku. Na vita yote itakapokwisha, nitaipata raha kwake.

 

3. Mwokozi wangu, ninakufuata, furaha yako inanituliza. Na siku moja utakuja tena kunichukua huko kwako.