Digg StumbleUpon LinkedIn YouTube Flickr Facebook Twitter RSS Reset

118 NI MWOKOZI mzuri ninaye

image_pdfsauvegarder en PDF-Saveimage_printImprimer-Print

118

1. Ni Mwokozi mzuri ninaye, alikufa kunikomboa. Alitoa uzima wake kwa ajili ya watu wote.

Pambio:
Alikufa msalabani, alikufa msalabani. Kwa ajili ya dhambi zangu zote alikufa msalabani.

 

2. Aliacha makao juu, akafika ulimwenguni; aliteswa kwa’jili yangu na kunifungulia mbingu.

 

3.Dhambi zangu ali’chukua, kujitwika hukumu yangu, na alijeruhiwa ili aniponye na ‘nipa raha.

 

4. Bwana Yesu alifufuka, akarudi mbinguni kwake; na yuaja upesi tena achukue walio wake.

 

F.A. Graves

No comments yet.

Leave a Comment