110 MWAMBA ulio pasuka

1. Mwamba uliopasuka, ndani yako nijifiche! Maji yale, damu ile itokayo mbavu zako, iwe dawa ya kuponya roho yangu na ubaya!

 

2. Kazi za mikono yangu, haziwezi kukomboa. Hata ningelia sana na kutenda kazi nyingi, singeweza kuokoka, peke yako u Mwokozi.

 

3.Ndani yangu sina kitu, naushika msalaba. Uchi mimi, univike! Sina nguvu, ‘nichukue! Ni mchafu, unioshe! Wewe u Mwokozi wangu.

 

4. Kwa maisha yangu yote hata nitatoa roho, hata saa ya kuitwa mbele ya Mfalme wangu, mwamba uliopasuka, nijifiche ndani yako!

A.M. Toplady, 1776

Video hii wanaimba sauti moja ila maneno tafauti, hii ni version ya Tanzania